*Wasema itafungua mipango yao mipya ya msimu ujao
*Kuwasili leo kwa maji, Yanga kutua na ndege
WAKATI
watani wa jadi Simba na Yanga wakitarajia kukutana kesho, katika mchezo
wa kukamilisha Ligi Kuu Tanzania Bara, Uongozi wa Klabu ya Simba
umesema mchezo wake huo, utafungua mipango mipya ya usajili wa klabu
hiyo, kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi.
Timu hizo zinatarajia kupishana
njia kuwasili Dar es Salaam, zikitokea katika visiwa vya Zanzibar,
Unguja na Pemba walipokuwa wakijiandaa.
Ujio wa timu hizo unafanywa kwa siri kubwa, lakini MTANZANIA limebaini
kuwa watoto wa Jangwani, watawasili kwa kutumia usafiri wa Anga, tofauti
na wapinzani wao Simba, ambao wanataraji kuwasili jijini leo kwa
usafiri wa maji, huku wakitaraji kulakiwa na mashabiki tayari kuwavaa
wapinzani wao Yanga, ambao wana kisasi cha kulipa bao 5-0.
Akizungumza
na MTANZANIA jana, Ofisa Habari wa klabu hiyo, Ezekel Kamwaga alisema
watatumia mchezo huo, kuipima vyema Yanga na kujua waanzie wapi kusajili
wachezaji watakaokuwa na viwango vya hali ya juu.
Kamwaga
alisema mchezo huo utakuwa muhimu sana kwao, ukiachilia mbali masuala ya
kuibuka na ushindi kuna mambo muhimu, ambayo kocha wao Patrick Liewig
atakuwa na jukumu la kuyaangalia kwa ukaribu.
“Kuna mambo muhimu
ambayo kocha atayafanyia kazi siku hiyo, haya yatatusaidia katika
mchakato mzima wa usajili wa kikosi chetu kipya cha msimu ujao wa Ligi
Kuu Tanzania Bara,” alisema.
Kamwaga alieleza wameipa nafasi
mechi hiyo wakiwa na malengo yao husika, ndiyo maana mikakati mbalimbali
ya kuhakikisha wanashinda imefanyika na hilo ndilo wanalowahakikishia
mashabiki wao.
Presha kwa mashabiki wa mpira wa miguu nchini
imezidi kupanda, huku wengi wao wakisubiri mchezo huo kwa hamu, ambao
huvuta hisia za watu wengi hata kwa nchi jirani na Tanzania.
Hali
imezidi kuwa imara kwa upande wa matawi ya Yanga, ambapo matawi ya
klabu ya Simba ambayo yalikuwa yamegawanyika yameweza kuketi pamoja na
kuongeza nguvu, huku kukiwa na tambo za mabango mbalimbali ya
kukashifiana.
Halikadhalika tawi la Yanga Ubungo terminal,
limeweza kuwa na kikao jana, ambacho wao walikiita cha siri kwa ajili ya
kumuua mnyama na kupeleka hamasa uwanjani.
Source: Mtanzania
Saturday, May 18, 2013
SIMBA: MECHI NA YANGA ITASAJILI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment